Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango leo Octoba 11, 2023 amefungua Mkutano wa Kimataifa wa Zao la Korosho unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es salaam.
Mkutano huo umejumuisha zaidi ya wadau 500 kutoka nchi 33 zinazozalisha na kula korosho, unatarajiwa kuchukua siku tatu na kumalizika Octoba 13, ambapo mada mbalimbali zinazohusu uendelezaji wa sekta ya Korosho kimataifa zitajadiliwa.
Naibu Waziri wa Kilimo David Silinde akimpokea Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip mpango, kwa ajili ya kufungua Mkutano wa Kimataifa wa Zao la Korosho unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es salaam (Tarehe 11-13 Oktoba 2023).
Akizungumza katika mkutano huo, Dkt. Mpango ametoa wito kwa Wizara ya Kilimo kuhakikisha kuwa inafikia azma ya kubangua korosho zinazozaliswa nchini badala ya kusafirisha nje ya nchi zikiwa ghafi, lengo ambalo linatakiwa kutimia ifikapo mwaka 2026.
Amesema kuendelea kuuza korosho isiyochakatwa (ghafi) kunasababisha kupunguza ajira za watanzania, kupunguza mapato ya fedha za kigeni pamoja na upatikanaji wa bidhaa zitokanazo na zao la korosho kama vile maziwa, mvinyo, juisi na mafuta.
Makamu wa Rais amesema ni muhimu mkutano huo ukajadili na kubadilishana uzoefu wa namna ya kuimarisha huduma za ugani na utoaji pembejeo kwa wakati ili kuongeza uzalishaji wa zao la Korosho, ambalo ni moja ya mazao yanayoliingizia Taifa fedha za kigeni.
Mkutano huo wa siku tatu (Tarehe 11-13 Oktoba 2023) unashirikisha Zaidi ya wadau 500 kutoka nchi 33 zinazozalisha na kula korosho.
Pamoja na mambo mengine lengo la Mkutano huo ni kutangaza fursa za uwekezaji zilizoko katika mnyororo wa thamani wa zao la korosho.
WANANCHI WA MABOGINI WANUFAIKA NA MRADI WA RISE
MOSHI-KILIMANJARO Wananchi wa kijiji cha Mabogini, kata ya Mabogini, wilayani Moshi Mkoani…










