MWANDISHI WETU, KILWA
Serikali imewataka wananchi kutumia boti ya kisasa ya Utalii ili kukuza utalii wa ndani.
Kauli hiyo ameitoa Waziri wa Maliasili na Utalii Mohamed Mchengerwa akiwa Kilwa Masoko kwenye hafla ya uzinduzi wa boti maalum ya Utalii ijulikanayo kama TAWA SEA CRUISER inayomilikiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA).
Mchengerwa amefafanua kuwa boti hiyo itakuwa ikifanya safari katika ukanda wote wa Pwani ili wajionee vivutio mbalimbali vya utalii.
Amevitaja baadhi ya vivutio vya utalii vinavyopatikana katika eneo la Kilwa kuwa ni pamoja na misitu ya matumbawe, kasa, mikoko, na samaki wa aina mbalimbali.
Katika hatua nyingine ametembelea maeneo ya kitalii ya mji mkongwe wa kihistoria wa Kilwa na kujionea vivutio vya utalii vya asili kama msikiti wa Karne ya 12 magofu ya kale na jumba la mfalme.
Akiwa katika msikiti wa kale ameiagiza Bodi ya TAWA kuona namna ya kuboresha mji huo ili kuvuta watalii wengi.
WANANCHI WA MABOGINI WANUFAIKA NA MRADI WA RISE
MOSHI-KILIMANJARO Wananchi wa kijiji cha Mabogini, kata ya Mabogini, wilayani Moshi Mkoani…











